KWA mara nyingine Ligi
Kuu nchini Uingereza inafikiria wazo la kucheza baadhi ya mechi zao nje
ya nchi hiyo. Dhana ya kucheza mechi 39 iliondolewa mwaka 2008 kufuatia
utata na upinzani mkali uliojitokeza. Lakini vilabu sasa vinaelekea
kukubali kucheza baadhi hizohizo 38 za mzunguko wa ligi zilizokuwepo
kuchezwa nje ya nchi. Mazungumzo bado yanaendelea lakini mapendekezo
hayo yanaweza kuzaa matunda katika miaka 10 ijayo. Vilabu vikubwa nchini
Uingereza vinataka kuongeza umaarufu wa ligi hiyo nje ya nchi kufuatia
mahudhurio makubwa katika mechi za kirafiki walizocheza nchini Marekani
kiangazi hiki ambapo mchezo wa Manchester United dhidi ya mabingwa wa
Ulaya Real Madrid uliochezwa huko Michigan uliingiza mashabiki
109,318. Ligi Kuu
pia
inashawishika kufanya hivyo kufuatia Ligi ya Mpira wa Kikapu nchini
Marekani-NBA na Ligi ya Mpira wa Miguu wa Kimarekani-NFL kucheza baadhi
ya mechi zao nchini Uingereza katika msimu ya karibuni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni