MENEJA wa zamani wa
Manchester United Sir Alex Ferguson amesisitiza kuwa walikuwa
wakielewana vyema na Shinji Kagawa wakati wakiwa wote klabuni hapo
lakini pamoja na hayo ameunga mkono uamuzi wa kiungo huyo kurejea katika
klabu yake ya zamani ya Borussia Dortmund. Ferguson alimsajili kiungo
huyo wa kimataifa wa Japan kutoka Dortmund katika kipindi cha usajili wa
kingazi mwaka 2012 na pamoja na kuonyesha uwezo wake kiasi wakati wa
msimu wake wa kwanza Old Trafford, Kagawa alishindwa kabisa kuingia
katika mipango ya David Moyes wakati Ferguson alipoondoka kabla ya
kuamua kurejea Dortmund. Ferguson amesema hajawahi kupoteza imani juu ya
uwezo wa Kagawa kung’aa katika Ligi Kuu lakini anaamini nafasi ya nyota
huyo mwenye umri wa miaka 25 iliingia matata muda mfupi baada ya
kusajiliwa kwa Juan Mata kutoka Chelsea Januari mwaka jana. Kocha huyo
mkongwe aliendelea kudai kuwa alikuwa na furaha alipokuwa na Kagawa
kwani alizoea mapema mazingira lakini kila kocha ana mbinu zake na Moyes
alipomnunua Mata, nyota huyo aliona kama sio chaguo la kwanza tena ndio
maana anaona alifanya uamuzi sahihi wa kurejea mahali ambapo atajisikia
nyumbani.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 8 Oktoba 2014
KAGAWA ALIFANYA UAMUZI SAHIHI KUREJEA DORTMUND - FERGUSON.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni