MCHEZAJI wa zamani wa
kimataifa wa Hispania Luis Suarez anaamini kuwa Edinson Cavani anapaswa
kuondoka Paris Saint-Germain-PSG kwasababu siku ataendelea kuwa chaguo
la pili mbele ya Zlatan Ibrahimovic. Matajiri hao wa Ufaransa walitoa
kitita cha euro milioni 64.5 kwa ajili ya Cavani akitokea Napoli katika
majira ya kiangazi mwaka 2013na mshambuliaji huyo wa kimataifa wa
Uruguay amefunga mabao 25 katika mechi 43 alizocheza katika msimu wake
wa kwanza PSG pamoja na kucheza pembeni ili kumpa nafasi Ibrahimovic
kuchezeshwa katikati. Cavani amaekuwa akipata muda mwingi wa kucheza
katika nafasi yake ya ushambauliaji wa kati msimu huu kwasababu ya
kukosekana kwa Ibrahimovic aliyekuwa majeruhi lakini ameshindwa kufunga
mabao kama ilivyotegemewa. Kumekuwa na tetesi kuwa nyota huyo mwenye
umri wa miaka 27 anataka kuikacha timu hiyo na Suarez anafikiri itakuwa
hatua nzuri kuchukua kwa mustakabali wake. Suarez amesema anafikiri
Cavani anapswa kuondoka kwasababu Ibrahimovic ni mchezaji imara na
aliyekamilika zaidi yake hivyo ziku zote ataendelea kucheza nyuma yake.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 8 Oktoba 2014
CAVANI ANAPSWA KUHAMA PSG - SUAREZ.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni