Kipa
Iker Casillas amesema aliamua kukaa kimya, kutojibizana na aliyekuwa
kocha wake, Jose Mourinho sababu ya kulinda maslahi ya Real Madrid.
Akijibu
swali aliloulizwa na mwandishi Iñaki Gabilondo katika mahojiano maalum,
Casillas alisema haikuwa sahihi kuzozana na Mourinho huku akijua
inayoathirika zaidi ni Madrid.
“Ningeweza kumjibu Mourinho, nilinyamaza kwa manufaa ya klabu. Sikuona kama ni sahihi kuwasha moto ambao ungeuunguza klabu.
“Hatukuwa tukizungumza vizuri hata kwenye mikutano ya waandishi tulienda wote, lakini hatukuzungumza.
“Mwanzo sikujua kama walikuwa na matatizo na mimi, lakini nilipoumia ndiyo nikagundua kuna kitu.
“Kwani hata baada ya kurudi kutoka majeruhi, kila siku msaidizi wake aliendelea kusema sikuwa fiti na mashindano.
“Taratibu nilianza kugundua kuna kitu kati yetu, mwisho nikagundua ni tatizo,” anafafanua Casillas.
Kipa
huyo aliingia katika hali ya kutoelewana na Mourinho wakati akiwa kocha
wa Madrid na alikuwa kocha wa kwanza kuanza kumtupa benchi nahodha huyo
wa Hispania.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni