MENEJA wa klabu ya
Arsenal, Arsene Wenger amepuuzia mzozo wake na meneja wa Chelsea Jose
Mourinho wakati kikosi chake kilipotandikwa mabao 2-0 katika mchezo wa
Ligi Kuu jana. Wawili hao walikwaruzana baada ya mshambuliaji wa Arsenal
Alexis Sanchez kukwatuliwa na Gary Cahill wa Chelsea katikati ya
kipindi cha pili ambapo Wenger alimsukuma Mourinho kifuani. Wawili hao
walitenganishwa na kamisaa wa mchezo huo Jonathan Moss ambapo ingawa
Wenger anaweza kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa tukio lake hilo
mwenyewe amelipa uzito mwepesi wakati akihojiwa. Wenger aliwaambia wana
habari kuwa hajutii kiti alichofanya kwani haoni kosa lake kwani alizuia
kwenda alipotaka bila sababu yoyote. Wenger amesema alichokuwa akitaka
yeye ni kwenda kumuangalia mchezaji wake aliyeangushwa chini lakini
Mourinho akamzuia ndio maana ikatokea kutoelewana baina yake lakini
katika mpira jambo hilo ni la kawaida. Kwa upande wake Mourinho amesema
alimzuia Wenger kwakuwa alijua anakata kumshinikiza mwamuzi kutoka kadi
nyekundu kwa faulo aliyocheza Cahil.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 7 Oktoba 2014
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni