CHIPUKIZI Calum Chambers
ameitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha wakubwa cha timu ya taifa
ya Uingereza baada ya John Stones kulazimika kujitoa kutokana na
majeruhi. Beki huyo wa klabu ya Arsenal, alikuwa ameitwa katika kikosi
cha timu ya taifa cha vijana chini ya umri wa miaka 21 kinachonolewa na
Gareth Southgate kwa ajili ya mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya mwakani
dhidi ya Croatia. Lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 19 sasa
amejumuishwa katika kikosi cha Roy Hodgson kuelekea katika mechi za
kufuzu michuano ya Ulaya mwaka 2016 dhidi ya San Marino na
Estonia. Stones amejitoa kufuatia kuumia kifundo cha mguu katika mchezo
dhidi ya Manchester United ambao Everton walitandikwa kwa mabao
2-1. Kutokana na hilo Chama cha Soka cha Uingereza-FA kilitoa taarifa ya
Hodgson kumchukua Chambers kutoka katika kikosi cha
Southgate. Uingereza itakwaana na San Marino katika Uwanja wa Wembley
Alhamisi hii kabla ya kuivaa Estonia huko Tallinn siku tatu baadae.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 7 Oktoba 2014
CHAMBERS AITWA KIKOSI CHA UINGEREZA KUZIBA NAFASI YA STONES.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni