Taifa
Stars itapambana vilivyo bila ya kuwa na mshambuliaji wake Mbwana
Samatta wakati inaivaa Benin katika mechi ya kirafiki Jumamosi jijini
Dar es Salaam.
Stars inacheza mechi hiyo ya kirafiki dhidi ya Benin ikiwa chini ya kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa.
Samatta aliumia katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya nusu fainali dhidi ya Setif ya Algeria.
Habari za uhakika kutoka katika kambi ya Stars jijini Dar zinaeleza kuwa Samatta amebaki DR Congo akitibiwa.
"Kweli Samatta hajaingia kambini, sisi tayari tunaendelea na mazoezi," alisema mmoja wa wachezaji.
Wachezaji
wengine wa Stars wanaocheza nje ya Tanzania kama Thomas Ulimwengu,
Mwinyi Kazimoto na Juma Luizio wameishajiunga na kikosi hicho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni