WINGA wa zamani wa klabu
za Arsenal na West Ham United, Freddie Ljungberg amesema Ligi Kuu mpya
iliyoanzishwa nchini India itakuwa na mafanikio. Ljungberg mwenye umri
wa miaka 37 anatarajiwa kucheza sambamba na mshambuliaji wa zamani wa
Arsenal na Chelsea Nicolas Anelka mwenye umi wa miaka 35 katika timu ya
Mumbai City inayonolewa na meneja wa zamani wa Sunderland Peter
Reid. Akihojiwa Ljungberg ambaye amewahi kushinda mataji mawili ya Ligi
Kuu akiwa na Arsenal amesema katika mchezo wao kwanza wanatarajiwa
kuwepo mashabiki wapatao 110,000 hivyo hiyo ni dalili nzuri ya kuonyesha
mafanikio katika ligi hiyo. Ligi Kuu nchini India inatarajiwa kuanza
kutimua vumbi Octoba 12 mwaka huu na itadumu ka kipindi cha wiki
10. Nyota waliowahi kushinda Kombe la Dunia akiwemo Alessandro Del
Piero, Marco Materazzi, David Trezeguet na Robert Pires ni miongozi mwa
wachezaji wenye majina makubwa watakaocheza katika ligi hiyo kwa
madhumuni ya kuiongezea umaarufu.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 7 Oktoba 2014
LIGI KUU YA INDIA ITAFANIKIWA - LJUNGBERG.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni