STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 24 Oktoba 2014

CHID BENZ ANASWA NA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE DAR

CHID BENZ
Msanii maarufu wa Hip Hop nchini, Chid Benz ameshikwa akiwa na bangi na madawa ya kulevya.

Chid Benz ambaye jina lake halisi ni Rashidi Abdallah Makwiro, ameshikwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Habari za ndani zimeeleza Chid Benz ameshikwa akiwa na kete 12 za madawa aina ya heroine wakati akiwa njiani kwenda kufanya shoo mjini Mbeya.
Shoo hiyo ya Instagram Party ilipangwa kufanyika kesho mjini Mbeya.
Kamanda wa Kuthibiti na kupambana na Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa amethibitisha kukamatwa kwa Chid Benz.
“Kweli tumemkamata bwana Rashidi Makwiro maarufu kama Chid Benz akiwa na kete kumi na mbili pamoja na misokoto ya bangi.
“Tunamshikilia kwa mahojiano maalum, lakini hauwezi kueleza sehemu alipo kwa sasa,” alisema Nzowa.
Chid Benz ni kiongozi wa kundi la La Familia lenye makazi yake Ilala jijini Dar.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox