KLABU ya Manchester
United ina uhakika kuwa Angel Di Maria atakuwa fiti kwa ajili ya mchezo
wa Jumapili dhidi ya Chelsea pamoja na kupata majeruhi katika mchezo wa
jana dhidi ya West Ham United. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina
alikwua akisikia maumivu katika kifundo cha mguu na kutolewa nje katika
dakika ya 76 ya mchezo huo huku akionekana kuwekea barafu katika eneo
hilo wakati akiwa benchi. Hata hivyo imedaiwa kuwa Di Maria amefanyiwa
vipimo katika uwanja wa mazoezi wa United leo kwa ajili ya tahadhari
lakini nyota huyo wa zamani wa Real Madrid anatarajiwa kuwa fiti katika
mchezo dhidi ya Chelsea. Di Maria mwenye umri wa miaka 26 amekuwa katika
kiwango bora toka atue Old Trafford ambapo tayari ameshatengeneza
nafasi nne katika mechi sita huku akitengeneza nafasi ya bao alilofunga
Marouane Fellaini katika mchezo wa jana uliomalizika kwa sare ya mabao
2-2.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 21 Oktoba 2014
DI MARIA ATAKUWA FITI KUIVAA CHELSEA - UNITED.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni