NAHODHA wa zamani wa
klabu ya Manchester United, Roy Keane amedai alipewa ofa ya kupewa jezi
maarufu ya namba saba katika klabu hiyo na aliyekuwa meneja Sir Alex
Ferguson ili kuzia David Beckham kuipata jezi hiyo. Keane ambaye
aliondoka United mwaka 2005 baada ya kuitumikia kwa miaka kadhaa
alibainisha hayo katika kitabu chake kipya kiitwacho The Second Half
ambacho kimeanza kuuzwa katika mitaa mbalimbali ya jiji la Manchester
kabla ya muda wake halisi wa kutoka. Kwa mujibu wa Keane baada ya nguli
wa zamani wa Ufaransa Eric Cantona kuondoka klabuni hapo mwaka 1997,
Ferguson alikuwa hataki kumpa Beckham jezi hiyo ambayo imevaliwa na
manguli kama Bryan Robson na George Best huku baadae Cristiano Ronaldo
akiivaa. Katika kitabu hicho Keane amekaririwa akidai kuwa katika United
namba saba ni namba ya kipekee hivyo wakati Cantona alipondoka kulikuwa
na mjadala nani apewe jezi ya namba hiyo tena. Keane aliendelea kudai
kuwa Ferguson alimvuta ofisini kwake na kumwambia anataka aivae jezi
namba saba kwani anajua Beckham ataitaka nay eye hakupenda kumpa lakini
alikataa ombi hilo. Hata hivyo baada ya Keane kukataa, Beckham alikuja
kupewa jezi hiyo baada ya kuelewana vyema na Ferguson mpaka uhusiano wao
ulipokuja kuyumba mwishoni na kupelekea Beckham kutimkia Real Madrid ya
Hispania. Keane aliitumikia United kwa kipindi cha miaka 12, nane kati
ya hiyo akiwa nahodha na kufanikiwa kushinda mataji saba ya Ligi Kuu,
manne ya Kombe la FA na Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 1999.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 8 Oktoba 2014
FERGUSON ALITAKA KUNIPA JEZI NAMBA 7 BADALA YA BECKHAM - KEANE.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni