DEREVA nyota wa
mashindano ya langalanga kutoka timu ya Force India, Sergio Perez amedai
kuwa ajali iliyomuacha dereva Jules Bianchi na majeraha ya kichwa,
haikubali na iliweza kuepukika. Perez ambaye ni raia wa Mexico amesema
madereva lazima watalitaka shirikisho la mashindano hayo-FIA kutaka
ufafanuzi wa kile kilichotokea na hatua zitachukuliwa kuepuka hali
hiyo. Perez aliendelea kudai kuwa wanapaswa kupewa majibu ya kina wa
kitu gani haswa kilitokea katika ajali hiyo mbaya. Bianchi kwasasa
anaendelea vyema ingawa bado yuko katika chumba cha uangalizi maalumu
baada ya gari lake kupoteza mwelekeo na kuligonga trekta lililokuwa
pembezoni wakati mashindano ya Japan Grand Prix Jumapili
iliyopita. Perez amesema inatakiwa hatua mpya za makusudi zichukuliwe
ili kuwepo na gari la usalama popote ambapo trekta linatumika kwa ajili
ya kuondoa magari yaliyopata hitilafu lkatika mashindano hayo ili
kuepuka kujirudia kwa ajali kama hiyo.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 9 Oktoba 2014
MADEREVA WA LANGALANGA WATAKA MAELEZO KUFUATIA AJALI YA BIANCHI.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni