MSHAMBULIAJI nyota wa
klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amebainisha kuwa aliweka soka
lake hatarini kwa kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya
Atletico Madrid msimu uliopita pamoja na kusumbuliwa na majeruhi. Nyota
huyo wa kimataifa wa Ureno alikutwa na tatizo hilo mwishoni mwa msimu wa
2013-2014 lakini halikumzuia kutocheza mchezo huo walioshinda mabao 4-1
dhidi ya Atletico huku yeye akifunga bao moja. Hata hivyo Ronaldo sasa
amekiri kuwa ilikuwa bora zaidi kwa mwili wake kupumzika badala ya
kucheza mchezo huo. Ronaldo amesema ni kweli alijiweka katika hatari kwa
kucheza fainali hiyo iliyochezwa jijini Lisbon lakini katika maisha
huwezi kushinda kitu kama muda mwingine hutaweza kujiweka katika
hatari. Nyota huyo aliendelea hakuna mchezaji anayependa kukosa fainali
ya Ligi ya Mabingwa au michuano ya Kombe la Dunia ndio maana alijisukuma
hivyohivyo na kuamua kucheza. Hata hivyo Ronaldo amesema jitihada zake
zililipa kwa kushinda taji la Ligi ya Mabingwa huku akifunga bao lakini
mambo hayakwenda akiwa na timu ya taifa ya Ureno kwani walienguliwa
mapema.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 9 Oktoba 2014
NILIHATARISHA SOKA LANGU KWA AJILI YA FAINALI YA LIGI YA MABINGWA - RONALDO.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni