CHAMA cha Wachezaji Soka
wa Kulipwa-PFA kimeponda mpango wa Ligi ya Soka nchini Uingereza
kutumia viwanja vyenye nyasi bandia katika ligi daraja la kwanza na
pili. Ofisa mkuu msaidizi wa PFA, Simon Barker amesema wameshangazwa na
kusikitizshwa na uamuzi uliotolewa hivi karibuni. Barker aliendelea
kudai kuwa wakiwa kama wawakilishi wa wachezaji walipaswa kushirikishwa
katika maamuzi hayo kabla ya wenyeviti wa vilabu hawajatoa uamuzi kwani
wanaocheza katika viwanja ni wajumbe wao. Kiongozi huyo wa PFA aliongeza
kuwa Chama cha Mameneja wa Ligi pia hakikushirikishwa na kuongeza
wasiwasi juu ya majeruhi na athari zitakazotokea wakati wakitumia
viwanja hivyo. Mapema Septemba mwaka huu wenyeviti 26 kati ya 46 wa
vilabu walikubalia mpango huo mpya wa viwanja vya nyasi za bandia
mapendekezo ambayo yanatarajiwa kupitishwa katika mkutano mwingine
Novemba.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 9 Oktoba 2014
PFA YALALAMIKIA VIWANJA VYA NYASI BANDIA KATIKA LIGI ZA CHINI.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni