SHIRIKISHO la Soka
nchini Brazil-CBF limedai kuwa limemtema kiungo wa Chelsea Ramires
katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo kwa ajili ya mchezo wa
kirafiki wa kimataifa dhidi ya Argentina na Japan na nafasi yake
itachukuliwa na Souza anayecheza klabu ya Sao Paulo. CBF imedai kuwa
Souza mwenye umri wa miaka 25 ambaye ni kiungo wa ulinzi ataungana na
mchezaji mwingine ambaye ameitwa kwa mara ya kwanza golikipa wa Gremio
Marcelo Grohe. Ramires ameachwa kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya
misuli. Grohe, ambaye hajafungwa katika mechi nane mfululizo akiwa na
Gremio, amechukuliwa kama tahadhari baada ya golikipa chaguo ka kwanza
Jefferson kuumia kidole wakati akiitumikia klabu yake ya
Botafogo. Brazil itakwaana na Argentina jijini Beijing Octoba 11 na
baadae kuivaa Japan nchini Singapore siku tatu baadae.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 3 Oktoba 2014
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni