MENEJA wa klabu ya
Liverpool, Brendan Rodgers ameonyesha kuwahusudu Cristiano Ronaldo na
Gareth Bale kuelekea katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya
Real Madrid. Rodgers amesema anaamini kuwa wawili hao wangepata
mafanikio katika mashindano ya riadha ya olimpiki kama wangeamua kufanya
kazi tofauti. Liverpool inahitaji matokeo mazuri katika mchezo wao huo
wa Jumatano utakaofanyika Anfield baada ya kupata kipigo cha kushtusha
katika mchezo uliopita dhidi ya FC Basel. Pamoja na hayo Rodgers ameonya
kuwa haitakuwa kazi rahisi kwa timu yake kupata matokeo wanayohitaji
kutokana vipaji vya mchezaji mmoja mmoja walivyo navyo Madrid. Rodgers
amesema Madrid wana vipaji vya hali ya juu na jinsi wanavyocheza
inawafanya kuwa timu hatari kukutana nayo. Madrid kwasasa ndio
wanaoongoza kundi B wakiwa na alama sita kutokana na michezo miwili
waliyocheza Liverpool wako nafasi ya pili wakikabana koo na Basel wote
wakiwa na alama tatu.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumanne, 21 Oktoba 2014
Home
/
Unlabelled
/
RONALDO NA BALE WANGEWEZA KUWA MABINGWA OLIMPIKI KAMA WANGEAMUA KUWA WANARIADHA - RODGERS.
RONALDO NA BALE WANGEWEZA KUWA MABINGWA OLIMPIKI KAMA WANGEAMUA KUWA WANARIADHA - RODGERS.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni