MSHAMBULIAJI nyota Luis
Suarez anatarajiwa kuanza kuitumikia Barcelona kwa mara ya kwanza wakati
vinara hao wa La Liga wataposafiri kuifuata Real Madrid katika mchezo
wa kwanza wa el Clasico utakaochezwa kesho. Suarez alikuwa ameruhusiwa
kucheza baadhi ya mechi za kirafiki kwa klabu ya nchi yake toka
aliposajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 75 akitokea Liverpool baada
ya kufungiwa miezi minne kwa kosa la kumng’ata beki wa Italia Giorgio
Chiellini katika Kombe la Dunia Juni mwaka huu. Nyota huyo wa kimataifa
wa Uruguay, anatarajiwa kucheza mechi yake hiyo ya kwanza katika Uwanja
wa Santiago Bernabeu akiwa sambamba na Neymar na Lionel Messi. Ujio wa
Suarez unaweza kufunikwa na Messi ambaye amebakisha bao moja kuifikia
rekodi ya mabao 251 katika La Liga iliyowekwa na Telmo Zarra aliyechezea
Atletico Bilbao kati ya mwaka 1940 mpaka 1955. Kiungo wa Barcelona,
Andres Iniesta ana matumaini wachezaji wote hao wawili yaani Messi na
Suarez wanatang’ara katika mchezo huo ili kuendeleza rekodi yao nzuri ya
kushinda Bernabeu ambapo mpaka sasa wameshashinda mechi nne kati ya
sita walizokutana katika uwanja huo.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 24 Oktoba 2014
SUAREZ KUANZA KUITUMIKIA BARCELONA KWA MARA YA KWANZA KATIKA EL CLASICO KESHO.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni