STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 24 Oktoba 2014

LUIS VAN GAAL AMSOGEZA KIPA VICTOR VALDES OLD TRAFFORD BAADA YA KUWA HURU AKITOKEA BARCELONA.

KIPA wa zamani wa Barcelona Victor Valdes ameanza Mazoezi na Manchester United baada ya kuwa nje kwa muda mrefu akipona Goti lake aliloumia vibaya.
Valdes, mwenye Miaka 32, aliumia Goti hilo Mwezi Machi na kulikosa Kombe la Dunia kuichezea Nchi yake Spain.
Kabla ya kuumia, Valdes alikuwa ameshatoa uamuzi wa kuondoka Barcelona mwishoni mwa Msimu uliopita baada ya kukataa kuongeza Mkataba wake uliokuwa ukimalizika.
Inasemekana Meneja wa Man United, Louis van Gaal, ndie aliemkaribisha Valdes kufanya Mazoezi na Klabu yake wakati akiendelea kujiweka fiti baada ya kupona.
Taarifa kutoka Man United ilisema: “Valdes atakuwa chini ya uangalizi wa Madaktari wa Manchester United akiendelea kupona Goti lake wakati akisubiri kuanza Mazoezi na Timu ya Kwanza.”
Hata hivyo, Man United, ambae Kipa wake wa kwanza ni Mhispania David De Gea na Nambari mbili ni Anders Lindegaard, haijapasua kama itampa Mkataba Valdes.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox