STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 3 Desemba 2014

KHEDIRA ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI.

KIUNGO wa klabu ya Real Madrid, Sami Khedira ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya kulazwa kwa siku moja kwa uangalizi kutokana na mtikisiko katika ubongo jana wakati wa mchezo wa Kombe la Mfalme dhidi ya Cornella. Khedira aligongana na kiungo wa Cornella David Garcia muda mfupi baada ya mapumziko katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Santiago Bernabeu kabla ya kucheza kwa dakika chache na baadae kutolewa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Jese. Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo, Khedira alifanyiwa vipimo zaidi leo na kuruhusiwa lakini haijajulikana na muda gani atakaa nje ya uwanja. Madrid ambao ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo walitinga hatua ya timu 32 bora bada ya kushinda mchezo wao wa mkondo wa pili kwa mabao 5-1 dhidi ya timu hiyo ya daraja la tatu hivyo kuwafanya kusonga mbele kwa jumla ya mabao 9-1. Madrid sasa inakabiliwa na mchezo mwingine wa La Liga Jumamosi hii dhidi ya Celta Vigo huku wakiwa na matumaini ya kushinda na kuendelea pengo lao la alama mbili dhidi ya mahasimu wao Barcelona.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox