STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 5 Desemba 2014

MCHEZAJI WA GABON AFUNGIWA MECHI TATU URUSI KWA KUTOA ISHARA YA MATUSI BAADA YA KUBAGULIWA.

KIUNGO wa kimataifa wa Gabon, Guelor Kanga amefungiwa mechi tatu na Shirikisho la Soka la Urusi-RFU kwa kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Spartak Moscow ambao walimfanyia vitendo vya ubaguzi wa rangi. Kiungo huyo wa klabu ya FC Rostov mwenye umri wa miaka 24 alikuwa akipigiwa kelele za nyani na mashabiki wa Spartak wakati wa mchezo wa Ligi Kuu nchini humo uliofanyika jijini Moscow jana. Nyota huyo naye alijibu mapigo hatua ambayo RFU ilibidi kuchukua hatua kwa kumtoza pia na faini ya paundi 600. Spartak nao walitozwa faini ya paundi 830 kutokana na mashabiki wao kuonyesha vitendo vya kibaguzi. Septemba mwaka huu beki wa Dynamo Moscow Christopher Samba alifungiwa mechi mbili kwa kufanya tukio kama hilo wakati mashabiki wa timu ya Torpedo Moscow walivyomfanyia vitendo vya kibaguzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox