Alexis Sanchez akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la pili dhidi ya Stoke City jumapili iliyopita
GWIJI wa Arsenal, Thierry Henry
amemtabiria mazuri Alexis Sanchez akitangaza kuwa nyota huyo raia wa
Chile atakuwa mrithi wa kufumania nyavu Emirates.
Sanchez ameanza kwa makali katika msimu
wake wa kwanza wa ligi kuu England na siku ya jumapili iliyopita Arsenal
ikishinda 3-0 dhidi ya Stoke City alikuwa moto wa kuotea mbali na
alitia kambani gozi la ng'ombe.
Uwezo wake wa kumalizia pasi za
mwisho,kufunga na kasi yake ya umeme kumesababisha watu wamfananishe na
Henry, mshambuliaji mkubwa katika historia ya klabu hiyo. Mfaransa huyo
anaamini kumfananisha yeye na Sanchez ni sahihi.
Thierry Henry akishangilia bao la ushindi la Arsenal dhidi ya Leeds United katika mechi ya FA januari 2012
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni