MWANASOKA bora wa dunia na mshambuliaji wa Real Madrid na Ureno, Cristian Ronaldo angejilaumu mno kufuatia kukosa mkwaju wa penalti wakati Madrid ikiongoza kwa bao moja, lakini baadaye akawa shujaa kwa kufunga goli la tatu Real ikishinda 3-1 dhidi ya Malaga katika mechi ya ligi kuu Hispania iliyopigwa usiku huu uwanja wa Santiago Bernabeu.
Magoli mengine ya Real Madrid yamefungwa na Sergio Ramos na James Rodriguez, pasi zote zikitoka kwa CR7.
Nahodha wa Real Madrid, Sergio Ramos akishangilia goli na Cristiano Ronaldo
Sergio Ramos akishangilia goli alilofunga dakika ya 24 dhidi ya Malaga
James Rodriguez naye alicheka na nyavu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni