STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 25 Juni 2015

KIPA HUGO WA SPURS NJIANI KUTUA OLD TRAFFORD

Zipo ripoti nzito toka England zinazodai Meneja wa Manchester United Louis van Gaal na Kipa wa Tottenham Hugo Lloris wamefikia muafaka na Kipa huyo wa Kimataifa wa France ambae ameshakubaliana kuhusu maslahi yake binafsi huko Old Trafford. 

Huku kukiwa na mipango ya chini chini ya Kipa Nambari Wani David de Gea kurudi kwao Spain kuidakia Real Madrid, kumchukua Hugo Lloris kunaelekea kuziba pengo hilo.Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi, Gazeti linaloheshimika huko France L'Equipe, kilichobaki sasa ni mazungumzo ya kukubaliana Ada ya Uhamisho na Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy.
L'Equipe imedai Levy amemhakikishia Lloris kuwa Klabu yeyote itakayotoa Ofa ya Pauni Milioni 18 kwenda juu basi atamruhusu kuhama White Hart Lane.Lloris, mwenye Miaka 28, alijiunga na Tottenham Mwaka 2012 akitokea Lyon ya France kwa Dau la Pauni Milioni 11.4.
Hata hivyo, Levy anasifika mno kwa ugumu wa kutoa Wachezaji wake Nyota na kama akiwaruhusu basi Dau lao huwa sio masihara. 


Juan Mata

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox