STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 23 Julai 2015

BAADA YA KUTUA ANFIELD BENTEKE ANENA HAYA

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ubelgiji, Christian Benteke amesema kwamba ametua Liverpool kutoka Aston Villa ili kushinda mataji.

Benteke, aliyejiunga na timu ya Midlands mwaka 2012 na kuifungia mabao 42 katika mechi 88 za ligi, arrived aliwasili viwanja vya mazoezi vya Wekundu hao, Melwood Jumatano baada ya Liverpool kukamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 32.5.

Liverpool pia imewasajili washambuliaji Danny Ings kutoka Burnley, na Roberto Firmino kutoka Hoffenheim, ili kuirejeshea makali safu yao ya ushambuliaji inayomkosa wa muda mrefu, Daniel Sturridge na Luis Suarez aliyehamia Barcelona msimu uliopita na Raheem Sterling aliyetimkia Manchester City. 




Akizungumza mara baada ya kukamilisha uhamisho wake, Benteke alisema; "NIna furaha sana kuwa hapa na ningependa kumshukuru mmiliki, Ian (Ayre) na pia kocha kwa jitihada zao za kunifikisha hapa.

"Nafikiri ilikuwa klabu sahihi, kwa sababu nilikuwa nina mawasiliano mazuri na kocha na nilitaka kuwa sehemu ya mipango yake. 

"Nafahamu Liverpool ni habari kubwa. Wameshinda mataji mengi ya Ligi Kuu na matano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na pia Kombe la UEFA na mataji mengi. Nafahamu ni klabu kubwa.

Alipoulizwa ni kipi kinamhamasisha yeye kama mchezaji, alisema: "Ni juu ya kushinda mataji. Ni kuhusu kufanya kitu fulani katika kazi yangu ambacho naweza labda kuwaeleza wanangu nilichokifanya,".

WAPYA WALIOSAJILIWA LIVERPOOL 2015

Christian Benteke - Pauni Milioni 32.5 kutoka Aston Villa
Roberto Firmino - Pauni Milioni 29 kutoka Hoffenheim
Nathaniel Clyne - Pauni Milioni 12.5 kutoka Southampton
Joe Gomez - Pauni Milioni 3.5 kutoka Charlton
Danny Ings kutoka Burnley
James Milner kutoka Manchester City
Adam Bogdan kutoka Bolton

JUMLA IMETUMIA: 
Pauni Milioni 77.5 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox