Baada ya kufuzu vipimo Mshambuliaji Hamisi Kiiza amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba ya Dar es Salaam.
Kiiza ambaye ni mshambuliaji wa zamani wa Yanga aliwasili jana akitokea nchini Uganda kwa ajili ya vipimo na kumalizia mazungumzo na uongozi wa Simba.
Akiwa nchini, Kiiza alisema amekuja kufanya kazi na Simba ambapo mashabiki wengi wanatamani kumwona uwanjani ilikujua kama kasi yake itaendana na mikiki ya timu ambazo zimefanya usajili wa nguvu kama Yanga na nyinginezo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni