STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 22 Julai 2015

MUNTARI KUTIMKIA UTURUKI BAADA YA KUTEMANA NA AC MILAN




KIUNGO ‘mtukutu’, Sulley Muntari anaweza kutua kwa vigogo wa Uturuki, Besiktas.

Mkongwe huyo wa Ghana mwenye umri wa miaka 30 alitofautiana na klabu yake AC Milan msimu uliopita na kutemwa akiwa amebakiza mwaka mmoja katika Mkataba wake.

Muntari alijiunga na klabu hiyo kwa mkopo kutoka kwa mahasimu, Inter Milan Januari mwaka 2012 kabla ya soka yake kumfanya apewe Mkataba wa kamili.

Na tangu ameondoka Milan amekuwa akihusishwa na kuhamia England na Marekani, lakini tovuti ya Sky Sport imeandika, mchezaji huyo wa kimataifa wa Ghana anakwenda Besiktas.



Besiktas ipo katika mkakati wa kuboresha kikosi chake, ikiwa tayari imesajili tena winga wake wa zamani, Ricardo Quaresma kutoka FC Porto nab ado inatarajiwa kusajili majina mengine makubwa, akiwemo mshambuliaji wa Ujerumani, Mario Gomez kutoka Fiorentina na Muntari aliyefunga mabao mawili katika mechi 16 za Milan msimu uliopita.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox