STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 18 Julai 2015

PATASHIKA MICHUANO YA KAGAME KUFUNGULIWA LEO , ORODHA KAMILI YA MABINGWA TANGU 1974


KIPYENGA cha michuano ya 40 ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kinapulizwa leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kutakuwa na mechi tatu katika siku ya kwanza leo kwenye viwanja viwili tofauti, kwanza KMKM ya Zanzibar na Telecom ya Djibouti kuanzia Saa 8:00 mchana na baadaye wenyeji Yanga SC dhidi ya Gor Mahia ya Kenya Saa 10:00 jioni Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, muda ambao pia APR ya Rwanda itamenyana na Al Shandy ya Sudan Uwanja wa Karume.

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Joseph Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa michuano hiyo na mgombea huyo wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (CCM) atawasili muda mfupi kabla ya mechi rasmi ya ufunguzi wa Kagame ya 40 kuanza, kati ya Yanga na Gor. 

Michuano hiyo ina makundi matatu, A likijumuisha timu za Yanga SC, KMKM, Telecom na Gor Mahia wakati wenyeji wengine, Azam FC wapo Kundi C pamoja na Malakia ya Sudan Kusini, Adama City ya Ethiopia na KCCA ya Uganda na Kundi B kuna APR ya Rwanda, Al-Shandy ya Sudan, LLB AFC ya Burundi na Heegan FC ya Somalia.

Azam FC itafungua dimba na KCCA Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Saa 10: 00 jioni mchezo utakaotanguliwa na mechi nyingine kati ya Adama City na Malakia utakaonza Saa 8:00 mchana, wakati jioni Saa 10:00 Uwanja wa Karume, LLB AFC itamenyana na Hegaan FC.

Mabingwa wa michuano hiyo, El Merreikh ya Sudan hawakuja kutetea taji, kwa sababu wapo kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Washindi wa pili wa Ligi Kuu ya Sudan, El Hilal pia nao hawajaja kwa kuwa wapo kwenye hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika. 




ORODHA YA MABINGWA NA WASHINDI WA PILI KOMBE LA KAGAME
MwakaNchiBingwaMatokeoMshindi wa piliNchiMwenyeji





1974 TanzaniaSimbaAbaluhya Kenya Tanzania
1975 TanzaniaYoung Africans2–0Simba Tanzania Zanzibar
1976 KenyaLuo Union2–1Young Africans Tanzania Uganda
1977 KenyaLuo Union2–1Horsed Somalia Tanzania
1978 UgandaKampala City Council0–0*[C]Simba Tanzania Uganda
1979 KenyaAbaluhya1–0Kampala City Council Uganda Somalia
1980 KenyaGor Mahia3–2Abaluhya Kenya Malawi
1981 KenyaGor Mahia1–0Simba Tanzania Kenya
1982 KenyaA.F.C. Leopards1–0Rio Tinto Zimbabwe Kenya
1983 KenyaA.F.C. Leopards2–1ADMARC Tigers Malawi Zanzibar
1984 KenyaA.F.C. Leopards2–1Gor Mahia Kenya Kenya
1985 KenyaGor Mahia2–0A.F.C. Leopards Kenya Sudan
1986 SudanAl-Merrikh2–2*[D]Young Africans Tanzania Tanzania
1987 UgandaVilla1–0Al-Merrikh Sudan Uganda
1988 KenyaKenya Breweries2–0Al-Merrikh Sudan Sudan
1989 KenyaKenya Breweries3–0Coastal Union Tanzania Kenya
1990
Mashindano hayakufanyika[E]
1991 TanzaniaSimba3–0Villa Uganda Tanzania
1992 TanzaniaSimba1–1*[F]Young Africans Tanzania Zanzibar
1993 TanzaniaYoung Africans2–1Villa Uganda Uganda
1994 SudanAl-Merrikh2–1Express Uganda Sudan
1995 TanzaniaSimba1–1*[G]Express Uganda Tanzania
1996 TanzaniaSimba1–0Armée Patriotique Rwandaise Rwanda Tanzania
1997 KenyaA.F.C. Leopards1–0Kenya Breweries Kenya Kenya
1998 RwandaRayon Sports2–1Mlandege Zanzibar Zanzibar
1999 TanzaniaYoung Africans1–1*[H]Villa Uganda Uganda
2000 KenyaTusker3–1Armée Patriotique Rwandaise Rwanda Rwanda
2001 KenyaTusker0–0*[I]Oserian Kenya Kenya
2002 TanzaniaSimba1–0Prince Louis Burundi Zanzibar
2003 UgandaVilla1–0Simba Tanzania Uganda
2004 RwandaArmée Patriotique Rwandaise3–1Ulinzi Stars Kenya Rwanda
2005 UgandaVilla3–0Armée Patriotique Rwandaise Rwanda Tanzania
2006 UgandaPolice2–1Moro United Tanzania Tanzania
2007 RwandaArmée Patriotique Rwandaise2–1Uganda Revenue Authority Uganda Rwanda
2008 KenyaTusker2–1Uganda Revenue Authority Uganda Tanzania
2009 SudanATRACO1–0Al-Merrikh Sudan Sudan
2010
Mashindano hayakufanyikadagger[J]
2011 TanzaniaYoung Africans1–0Simba Tanzania Tanzania
2012 TanzaniaYoung Africans2–0Azam Tanzania Tanzania
2013 BurundiVital'O2–0A.P.R. Rwanda Sudan
2014 SudanAl-Merrikh1–0A.P.R. Rwanda Rwanda



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox