WOLFSBURG YADAI HAWANA MPANGO WA KUMUUZA DE BRUYNE.
MKURUGENZI wa michezo wa Wolfsburg, Klaus Allofs amesisitiza kuwa klabu hiyo haina mpango wowote wa kumuuza Kevin De Bruyne katika usajili wa majira haya ya kiangazi.
Manchester City ndio wanaonekana kumuwinda nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji huku mwenyewe akithibitisha mapema mwezi huu kuwa wakala ameshafanya mazungumzo na klabu hiyo.
Hata hivyo, Wolfsburg bado wameendelea na msimamo wao wa kutotaka kumuacha De Bruyne na Allofs amebainisha kuwa klabu hiyo inatarajia kuangalia uwezekano wa kumboreshea maslahi katika mkataba wake nyota huyo mwenye umri wa miaka 24.
Allofs amesema De Bruyne ana mkataba na Wolfsburg unaomalizika mwaka 2019 na tayari wameshatuma ujumbe kuwa hawana mpango wa kumuuza. Mkurugenzi huyo aliendelea kudai kuwa kikubwa wanachotizama hivi sasa ni kupitia upya mkataba wake na kuangalia jinsi ya kuuboresha zaidi.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 1 Julai 2015
WOLFSBURG YADAI HAWANA MPANGO WA KUMUUZA DE BRUYNE.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni