Meneja
wa klabu ya Bournemouth ya nchini Uingereza,Eddie Howe amesema maamuzi
yaliyofanywa kinyume na matarajio ya wengi katika mchezo waliopoteza
dhidi ya Liverpool hayasameheki.
Mapema mchezaji wa Bournemouth Tommy Elphick alikaribia kufunga lakini alinyimwa kwa kucheza vibaya.''Huwezi kupingana na maamuzi na mambo hayo yalitunyima alama muhimu'' alisema meneja wa Bournemouth mwenye miaka 37 Eddie Howe.
Howe alisema kuwa atajaribu kutizama nini kitafuatia kwa mwamuzi wa mchezo huo Craig Pawson pamoja na waaamuzi wasaidizi. Katika mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Anfield, Liverpool waliondoka na ushindi mwembamba wa goli 1 kwa bila lililofungwa na mshambuliaji mpya wa timu hiyo Christian Benteke.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni