Robin Van Persie na Luis Nani hivi sasa ni wachezaji halali wa klabu ya Fenerbahce ya Uturuki.
Wote wawili wametokea Manchester united na kujiunga na wababe hao.
Kutokana
na tukio la pili la mashambulizi ya kigaidi dhidi ya wachezaji wa
Fenerbahce limeleta wasiwasi mkubwa kwa nyota hawa wawili.
Hivi sasa mchezaji Mehmet Topal ameshambuliwa kwa risasi na waliotajwa kuwa ni magaidi.
Shukrani
kwa gari lake la gharama Mercedez G Class ambalo kiyoo chake ni bullet
proof kwa hiyo risasi haikumfikia. Lakini kama angekua anaendesha gari
la kawaida basi hivi sasa yangekuwa mengine.
Hii ni mara ya pili kwa Fenerbahce kushambuliwa na wanaotajwa kuwa ni magaidi.
Mara ya kwanza ilikua ni April 4 ambapo klabu hiyo ilikua inaenda kwenye mechi ya ligi dhidi ya Caykur Rizespor.
Kwasababu malengo ya watu hao ni timu ya Fernebache na wachezaji wake.
Robin Van Persie na Nani wapo kwenye wasiwasi mkubwa kwasababu ni mastaa wa club hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni