Hispania
imekuwa nchi ya kwanza kuwa na timu tano zilizofuzu katika hatua ya
makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya Valencia
kuwatungua Monaco kwa uwiano wa mabao 4-3 katika hatua ya mtoano.
Valencia
almaarufu Los Che, ambao walishika nafasi ya pili katika michuano hiyo
mwaka 2000 na 2001, wanaungana na timu nyingine za Uhisapania ambazo ni:
Barcelona, Real Madrid na Atletico Madrid, huku Sevilla ambao walishika
nafasi ya tano katika La Liga wameingia moja kwa moja baada ya kuibuka
mabingwa wa ligi ya Europa mapema kabisa mwaka huu.
Alvaro Negredo ndio shujaa wa Valencia baada ya kuwafungia goli muhimu la ugenini na kuwapa nafasi hiyo ya kufuzu licha ya kufungwa
2-1. Negredo alianza kufunga dakika ya nne kabla ya Andrea Raggi
kuwasawazishia wenyeji dakika ya 17 na Elderson Echiejile kufunga la
pili dakika ya 75.
Mshambuliaji
wa zamani wa Manchester City Alvaro Negredo akishangilia goli lake
muhumi la ugenini lililoiwezesha Valencia kuitupa nje Monaco na kufuzu
hatua ya makundi Klabu Bingwa Ulaya.
Wachezaji wa Valencia wakishangilia
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni