STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 26 Agosti 2015

REKODI YA HISPANIA LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA.....


Hispania imekuwa nchi ya kwanza kuwa na timu tano zilizofuzu katika hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya Valencia kuwatungua Monaco kwa uwiano wa mabao 4-3 katika hatua ya mtoano.

Valencia almaarufu Los Che, ambao walishika nafasi ya pili katika michuano hiyo mwaka 2000 na 2001, wanaungana na timu nyingine za Uhisapania ambazo ni: Barcelona, Real Madrid na Atletico Madrid, huku Sevilla ambao walishika nafasi ya tano katika La Liga wameingia moja kwa moja baada ya kuibuka mabingwa wa ligi ya Europa mapema kabisa mwaka huu.

Alvaro Negredo ndio shujaa wa Valencia baada ya kuwafungia goli muhimu la ugenini na kuwapa nafasi hiyo ya kufuzu licha ya kufungwa 2-1. Negredo alianza kufunga dakika ya nne kabla ya Andrea Raggi kuwasawazishia wenyeji dakika ya 17 na Elderson Echiejile kufunga la pili dakika ya 75. 

Mshambuliaji wa zamani wa Manchester City Alvaro Negredo akishangilia goli lake muhumi la ugenini lililoiwezesha Valencia kuitupa nje Monaco na kufuzu hatua ya makundi Klabu Bingwa Ulaya.


Wachezaji wa Valencia wakishangilia 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox