Kikosi cha Manchester united kimesafiri kwenda kucheza mchezo wa marudiano dhidi ya Club Brugge ambapo kwa mara nyingine tena kipa David De Gea ameachwa na kikosi hicho.
Taarifa nyingine zinasema kwamba De Gea hajaficha hamu yake ya kuhamia club yake ya nyumbani alipozaliwa ambapo ni Real Madrid.
Matukio haya yanayotokeaa yanapata moto sana kutokana na taarifa nyingine kwamba wakala wa De Gea yupo jijini Manchester tayari kwa ajili kushugulikia ishu ya De Gea.
Kutokana na siku chache kubaki, tutegemee taarifa yoyote kuhusu David De Gea kwasababu mchezaji huyu bora wa Manchester united kwa msimu uliopita anategemea kucheza na sio kukaa benchi tena.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni