Mabingwa wa kombe la FA, Arsenal watalazimika kuvuka mitaa na kuwafuata wapinzani wao wa Kaskazini mwa jiji la London Tottenham Hotspurs, kwa ajili ya kupambana kwenye mchezo wa mzunguko wa tatu wa kombe la ligi "CAPITAL ONE CUP"
Arsenal wameangukia kwa mahasimu wao baada ya chama cha soka nchini Uingereza FA kuendesha zoezi la upangaji wa ratiba ya mzunguko wa tatu wa michuano hiyo ambayo huchezwa kwa mfumo wa mtoano.
Michezo mingine ya hatua ya tatu ya kombe la ligi ambayo inatarajiwa kuwa na mvuto pamoja na ushindani ni kati ya Aston Villa ambao watakua nyumbani Villa Park dhidi ya mahasimu wao wa jiji la Birmingham,Birmingam City.
Ipswich Town watalazimika kusafiri hadi mjini Manchester kwenye dimba la Old Trafford kupambana na Manchester United, Crystal Palace wakichuana na Charlton, wakati mabingwa watetezi Chelsea wakipangiwa kupambana na Walsall huko Bescot Stadium.
Klabu ya Carlisle inayoshiriki ligi daraja la pili nchini Uingereza itakutana na majogoo wa jiji Liverpool kwenye uwanja wa Anfield, baada ya kufanya kazi kubwa ya kuichabanga Qpr mabao 2-1 katika mchezo wa mzunguko wa pili.
Kwa upande wa Manchester City wamepangiwa kukutana na Sunderland ambao watakua nyumbani Stadium of Light.
MICHEZO MINGINE:
Middlesbrough v Wolves
Norwich v West Brom
Hull v Swansea
Leicester v West Ham
Fulham v Stoke
Newcastle v Sheffield Weds
Reading v Barnsley or Everton
Preston v Bournemouth
MK Dons v Southampton
Michezo hii ya mzunguuko wa tatu imepangwa
kuchezwa Septemba 22
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni