Simba
iko katika hatua za mwisho kumalizana na mshambuliaji hatari kutoka
Senegal ambaye anatarajia kutua nchini ndani ya siku mbili zijazo.
Papa Niang, raia wa Senegal aliyezaliwa Desemba 5, 1988, sasa ana miaka 26 atatua nchini kumalizana na Simba.
Mara
ya mwisho alikuwa akiichezea CF Monana ya Gabon ambayo alijiunga nayo
akitokea Al Shaabab ya Kuwaita, moja ya timu tajiri katika Ukanda wa
Ghuba ya Uajemi.
Habari
za ndani ya Simba zinaeleza Niang anakuja nchi kumalizana na uongozi wa
Msimbazi baada ya kuwa imekubaliana naye kila kitu.
"Ni
kweli, kuna mtu alipewa kufanya kazi hiyo ya Niang na mambo yamekwenda
vizuri, sasa anakuja nchini na anamalizana na uongozi.
"Viongozi wamekuwa wakilishughulikia hilo kwa kasi kubwa ili kuwahi dirisha la usajili," kilieleza chanzo cha uhakika.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni