Manchester
City imekamilisha usajili wa nyota wa Valencia, Nicolas Otamendi kwa
dau la paundi milioni 32, huku kocha mkuu wa klabu hiyo, Manuel
Pellegrini akiamini kwamba amenunua beki bora zaidi kutoka Hispania.
Mlinzi huyo wa kimataifa wa Argentina alifuzu vipimo vya afya jana na kukubali kusaini mkataba wa miaka mitano.
Otamendi alikuwa akihusishwa kutua Manchester United na Real Madrid, lakini leo ametambulishwa rasmi na Manchester City.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni