STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 31 Desemba 2015

BAADA YA USHINDI WA JANA, BARCELONA YAVUNJA REKODI YA REAL MADRID


2341052_heroa

 


Klabu ya Barcelona ya nchini Hispania imefanikiwa kuvunja rekodi iliyowekwa na wapinzani wao wakubwa Real Madrid ambayo waliiweka mwaka 2014.
 
Real Madrid mwaka jana ilifanikiwa kufunga magoli 178 ambayo yalikuwa hayajawahi kufungwa na klabu yoyote katika historia ya klabu ya Hispania.
 
Awali kabla ya mchezo kati ya Barcelona na Real Betis, Barcelona ilikuwa na magoli 176 na baada ya kuibuka na ushindi wa goli nne kwa bila dhidi ya Real Betis sasa Barcelona ndiyo timu inayoongoza kwa kufunga magoli mengi kwa mwaka mmoja kwa kuwa na magoli 180 na kuiacha Real Madrid ikiwa na magoli 178.
 
Kati ya magoli 180, Lionel Messi amefunga magoli 48, Suarez 48 na Neymar 41 ambayo ni sawa na asilimia 75 ya magoli yote ambayo Barcelona imefunga.
 
Aidha katika mchezo huo, mchezaji bora wa dunia mara nne, Lionel Messi alifanikiwa kufikisha michezo 500 akiichezea Barcelona.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox