STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 10 Januari 2016

MTIBWA WAIVUA UBINGWA SIMBA, YAICHAPA KAMOJA TU...

SIMBA SC imevuliwa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi, baada ya kufungwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar katika mchezo wa Nusu Fainali uliofanyika Uwanja wa Amaan, Zanzibar jioni ya leo.
 
Shujaa wa Mtibwa Sugar FC leo alikuwa ni kiungo Ibrahim Rajab ‘Jeba’ aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 45 akimalizia mpira uliopanguliwa na kipa Peter Manyika baada ya shuti la mshambuliaji Hussein Javu anayecheza kwa mkopo kutoka Yanga SC.
 
Pamoja na kufungwa, Simba SC walicheza vizuri wakiongozwa na mkongwe Mussa Hassan Mgosi ingawa bahati haikuwa yao.
 
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/Yanga-vs-Mtibwa-znz-3.jpg
 

Kwa matokeo hayo, Simba SC watapanda boti kesho mapema asubuhi kurejea Dar ea Salaam, wakati Mtibwa Sugar itasubiri mshindi kati ya Yanga SC na URA ya Uganda usiku wa leo, ikutane naye katika Fainali Jumatano.

 
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Peter Manyika, Emery Nimuboma/Brian Majwega dk46, Mohammed Hussein 'Tshabalala', Hassan Isihaka, Juuko Murshid, Justice Majabvi, Awadh Juma/Said Ndemla dk46, Jonas Mkude, Mussa Mgosi/Ibrahim Hajib dk46, Danny Lyanga/Paul Kiongera dk76 na Mwinyi Kazimoto/Abdi Banda dk86.
 

Mtibwa Sugar; Said Mohammed, Shaaban Nditi, Ally Shomary, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Dickson Daudi, Salim Mbonde, Mohammed Ibrahim, Muzammil Yassin, Hussein Javu/Jaffar Salum dk68, Ibrahim Rajab ‘Jeba’/Vincent Barnabas dk80 na Shiza Kichuya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox