Niyonzima ameamua kuidai Yanga mshahara baada ya kuona klabu hio ikipata kigugumizi cha kumkabidhi barua ya kuvunja mkataba.
Yanga wamekuwa wazito kuvunja mkataba wa Niyonzima huku juhudi zikiendelea za kupata suluhu baina yao na mchezaji. Chanzo cha karibu na Niyonzima kimeuambia mtandao wa Soka360 kuwa Yanga inamtumia waziri mmoja ambaye ni mpenzi wa klabu hio kujaribu kupata suluhu.
Wakati huo huo, baada ya Yanga kumtema Haruna Niyonzima, wachezaji wengine wa kigeni wa klabu hio wameamua kugoma wakishinikiza kupewa nakala za mikataba yao.
Beki Vincent Bossou na kiungo mshambuliaji aliyesajiliwa hivi karibuni, Boubacar Issoufou Garba wamegoma kujiunga na timu hio visiwani Zanzibar hadi wakabidhiwe nakala za mikataba yao.
Chanzo: Soka360
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni