Watoza ushuru wa Uganda URA FC leo wameenza vyema michuano ya kombe la Mapinduzi kwa kuibuka na ushindi wa goli 3-1 mbele ya wenyeji wao JKU mchezo uliochezwa katika uwanja wa Amani visiwani Zanzibar.
Katika mchezo huo ulio shuhdi magoli matatu ya kipatikana katika kipindi cha kwanza kwa Mohammed Abdallah kuiandikia JKU goli la kwanza.
URA katika kipindi hicho cha kwanza waliandika magoli mawili kupitia kwa Oscar Agaba na Villa Orgamchan na kuipelka URA mapumziko wakiwa mbele kwa goli 2-1.
Katika kipindi cha pili kama safui ya ushambuliaji ya JKU wangekuwa makini wangesawazisha goli hilo lakini walijikuta wakipoteza nafasi mbili za kujipatia magoli.
URA wakicheza soka la malengo waliandika goli la tatu katika dakika ya 77 kupitia kwa Orgamchan na kuipa ushindi wa goli 3-1 URA mbele ya JKU.
URA watashuka tena uwanjani hapo siku ya jumatano kuikabili Simba SC katika mchezo wa pili kundi A, wakati Simba SC wanatarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza wa kundi A leo usiku katika uwanja huo wa Amani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni