STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 24 Machi 2016

HAINA UBISHI KIIZA NDIYE FOWADI BORA KWA SASA...........


 

NI ukweli uliowazi kwa sasa kuna ubishi kati ya pande mbili za timu hasimu Bongo; Simba na Yanga juu ya timu gani ina straika mkali kuliko nyingine.

Yanga wao wanajivunia uwepo wa Mzimbabwe wao, Donald Ngoma na Mrundi, Amissi Tambwe ambao hakika wamekuwa chachu ya ushindi kikosini hapo tanngu kuanza kwa msimu huu, lakini kwa Simba wanaonekana si lolote kwani silaha yao ni Ibrahim Ajib na Mganda, Hamisi Kiiza.

Ukweli mastaa wote unafanya poa na wamekuwa nguzo muhimu mpaka sasa ambapo kila timu ina nafasi ya kutwaa ubingwa wa msimu huu, ubora wao ukianzia kwenye vita ya kusaka ufungaji bora Ligi Kuu Bara mpaka sasa, ambako chati hiyo inaongozwa na Kiiza mwenye mabao 19, anafuatiwa na Tambwe kwa mabao 17 na wengine wanafuatia.

Championi imekata mzizi wa fitina na kura imeangukia kwa Kiiza kama fowadi bora tangu kuanza kwa msimu huu, huku Ngoma licha ya kuonekana mkombozi wa Wanajangwani, bado anasubiri hata kwa staa wa Azam, Kipre Tchetche.

Miongoni mwa vigezo vilivyozingatiwa ni wingi wa mabao na uwezo wa mchezaji katika kuchana nyavu bila kujali ni aina gani ya michuano, kura iliyowadondokea Kiiza, Kipre na Tambwe, lakini bado Kiiza anabaki juu katika wingi wa mabao kama mchanganuo wa ‘Top 5’ ya watupiaji bora.
 
                                Jeremiah Juma

Fowadi wa Tanzania Prisons anashika nafasi ya tano katika mafowadi bora mpaka sasa akiwa na mabao 11 katika michuano miwili aliyocheza; ligi kuu na Kombe la FA. Idadi hii imewashinda mastaa kibao wa Azam, Simba na Yanga wakiongozwa na Allan Wanga, Ibrahim Ajib, Danny Lyanga, Malim Busungu na Simon Msuva.
 
                         John Bocco, Ngoma

Nahodha wa muda mrefu wa Azam, John Bocco yupo ‘rank’ moja na Mzimbabwe, Donald Ngoma wa Yanga, wote wakiwa idadi sawa kwa mabao 15 kwenye michuano yote mitano waliyocheza msimu huu. 
 

Lakini kwa kigezo cha fowadi asiyechagua michuano, Bocco ni bora ya Ngoma kwani katika michuano mitano amefunga katika michuano minne mpaka sasa (ligi kuu mabao (8), Mapinduzi (2), Kombe la Shirikisho (2) na Kagame (2).

Ngoma katika michuano mitano ambayo Yanga imehusika msimu huu, amefanikiwa kufunga kwenye miwili tu; ligi kuu (13) na Ligi ya Mabingwa Afrika mabao mawili.
 
                            Kipre Tchetche

Ni wa tatu katika chati ya mafowadi bora mpaka sasa akiwa na mabao 17. Staa huyo wa Azam wikiendi iliyopita alidhihirisha ubora wake baada ya kupachika mabao matatu katika ushindi wa mabao 4-3 waliyovuna Azam mbele ya Wasauz, Bidvest na kutinga hatua ya pili ya Kombe la Shirikisho.

Katika michuano mitano ambayo Azam imehusika msimu huu, Muivory Coast huyo amefunga katika michuano minne (ligi kuu (mabao 9), Mapinduzi (1), Kagame (4), Shirikisho (4).
 
                           Amissi Tambwe

Heshima yake kubwa ni kupiga hat trick, anazo tano za ligi kuu katika misimu mitatu aliyokaa Bongo hii. Anashika nafasi ya pili akiwa amefunga mabao 20 katika michuano mitano ambayo Yanga imeshiriki msimu huu. 

Katika michuano hiyo, Mrundi huyo amefanikiwa kufunga katika michuano minne ambayo ni ligi kuu mabao 17, Mapinduzi (1), Kagame (1) na Ligi ya Mabingwa (1).
 
                                     Hamisi Kiiza;

Kuna rundo la sababu za kumfanya kuwa fowadi bora mpaka sasa. Kwanza ndiye mwenye mabao mengi tangu kuanza kwa msimu huu ambako amefunga mabao 23, mabao matatu zaidi ya anayemfuatia, Tambwe.

Pili, kati ya orodha ya wakali watatu wa juu, ndiye aliyeshiriki michuano michache zaidi. Mitatu tu, Kombe la FA, ligi kuu na Mapinduzi ambapo amefunga kwenye ligi kuu mabao 19 na manne kwenye FA, kwa mantiki iwapo angeshiriki mitano kama kina Ngoma na Kipre pengine angekuwa anachungulia mabao 30 kwa sasa.

Tatu, katika orodha hiyo, Kiiza pekee ndiye amefunga kwenye Kombe la FA tena akifunga mabao mawili-mawili kila mchezo mpaka Simba inatinga robo fainali.

                                   Hitimisho:
Kiiza anahitaji bao moja tu katika mechi sita za ligi kuu Simba ilizobakiza ili kuandikisha rekodi ambayo haijawahi kutokea kwenye soka la Tanzania. Bao hilo litamfanya kufikisha mabao 20, idadi ambayo kwa mujibu wa takwimu, hakuna mchezaji wa kigeni aliyewahi kuifikisha .

Mkenya, Boniface Ambani wa Yanga msimu 2008/09 alitwaa kiatu kwa mabao 18, Tchetche wa Azam 2012/13 alikuwa na mabao 17 wakati Mrundi Tambwe ndiye mwenye mabao mengi, alipokitwaa akiwa na mabao 19 msimu wa 2013/14 akiwa na Simba.

Kiiza atakuwa Mganda wa pili kuwa mfungaji bora baada ya Michael Katende wa Kagera Sugar afanye hivyo 2007/2008 alipomaliza ligi na mabao 11.  

                              www.mdosejr@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox