YANGA
SC imefanikiwa kwenda hatua ya 16 Bora michuano ya Ligi ya Mabingwa
Afrika kufuatia kuitoa APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2.
Yanga
SC leo imelazimishwa sare ya 1-1 na timu ya jeshi la Rwanda Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam – na kwa kuwa ilishinda 2-1 katika mchezo wa kwanza
mjini Kigali wiki iliyopita, inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa
3-2.
Yanga sasa watamenyana na mshindi wa jumla kati ya Al Ahly ya Misri na Recreativo de Libolo ya Angola katika hatua ya 16 Bora.
Katika
mchezo wa leo, APR ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya tatu
kupitia kwa Fiston Nkinzingabo aliyefumua shuti kali akimalizia pasi ya
Jean Claude Iranzi.
Yanga
walifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 28 kupitia kwa mshambuliaji
wake, Donald Dombo Ngoma aliyefumua shuti la kitaalamu baada ya pasi
nzuri ya kiungo Mzimbabwe mwenzake, Thabani Scara Kamusoko.
Kwa ujumla mchezo wa leo, Yanga walicheza kwa kujihami zaidi wakionekana dhahiri kutaka kuulinda ushindi wao wa ugenini.
Na APR ingeongeza juhudi kidogo tu, ingeweza kuwatia simanzi mashabiki wa nyumbani – lakini labda bahati haikuwa yao.
Kikosi
cha Yanga leo kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Mwinyi
Hajji, Kevin Yondan, Vincent Bossou, Pato Ngonyani, Deus Kaseke/Geoffrey
Mwashiuya dk70, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Haruna
Niyonzima/Simon Msuva dk65.
APR:
Jean Claude Ndoli, Rusheshangonga Michael, Rutanga Eric, Rwatubyaye
Abdul, Emery Bayisenge, Yannick Mukunzi, Fiston Nkinzingabo/Djihad
Bizimana DK46, Benedata Janvier/Bertrand Iradukunda dk88, Issa
Bigirimana, Iranzi Jean Claude na Patrick Sibomana
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumamosi, 19 Machi 2016
NGOMA AIPELEKA YANGA KWENYE HATUA INAYOFUATA, WAICHAPA APR JUMLA YA MABAO 3-2
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni