STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 11 Aprili 2016

HARAKATI ZA UJENZI WA UWANJA KUANZA RASMI BUNJU, HIKI HAPA KIKOSI KAZI PALE MSIMBAZI

RAIS wa klabu ya Simba ya Dar es Salaam, Evans Elieza Aveva amemteua Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Zacharia Hans Poppe (pichani kulia) kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Ujenzi wa Uwanja Bunju Complex.
http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2015/03/Hans-284x300.jpg

Katika taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa Simba, kazi kubwa ya Kamati hiyo itakuwa kuratibu shughuli zote za ujenzi wa Uwanja ikiwa ni pamoja na kutafuta fedha za ujenzi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Mbali na Hans Poppe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Aveva amemteua Salim Muhene, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji kuwa Makamu wa Mwenyekiti.

Katibu ni Issa Batenga wakati Wajumbe wa Kamati hiyo ni Ally Suru, ambaye Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Adam Mgoyi ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Crescentius Magori, Imani Kajula na Jerry Yambi.

Kamati hiyo inatarajiwa kukutana Waandishi wa Habari kuelezea mikakati yao juu ya majukumu waliyopewa.

Chanzo: Binzubery Sports

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox