Baada ya kutibua rikodi za kutopoteza
mchezo kwa Yanga SC na Azam FC, Coastal union leo wamezima ndoto ya
Simba SC kuiwakilisha Tanzania Bara katika michuano ya Kombe la
shirikisho Afrika Mwakani, baada ya kuwafunga goli 2-1.
Matumaini ya Simba SC kushiriki michuano
ya kimataifa mwakani yamebakia katika mbio za ubingwa wa ligi kuu,
ambapo anafukuzana kwa karibu na Azam FC na Yanga.
Katika mchezo wa leo wa kombe la TFF
uliochezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Coastal union
walikuwa wa mwanzo kupata goli kupiti kwa Yousuf Sabo kwa mpira wa
adhabu aliopiga moja kwa moja na kuiandika Coastal goli la uongozi
katika dakika ya 20.
Kuingia kwa goli hilo Simba SC
walijaribu kufika langoni mwa Coastal union bila mafanikio yoyote katika
kipindi cha kwanza na kuplekea dakika 45 za kwanza kumalizika kwa
Coastal union kuibuka na ushindi wa goli 1-0.
Kipindi cha Simba SC walianza kwa
mabadiliko ambapo aliingi Hamisi Kiiza na Awadh Juma kuchukuwa nafasi ya
Said NDemla na Justice Majabvi .
Mabadiliko hayo yaliongeza kasi kwa
Simba SC na katika dakika ya 49 Hamiisi Kiiza aliitendea vyema krosi ya
Ibrahim Ajibu na kuiandikia Simba SC goli la kusawazisha.
Kuingia kwa goli ilo kulipeleka kocha Ally Jangalu kumuinua kwenye benchi Ahmad Ally Shiboli na kuingia uwanjani.
Simba SC waliendelea kushambulia kwa kasi huku Coastal union wakitumia mipira ya kushtukiza kupitia kwa Shiboli na Mahadhi.
Katika dakika ya 84 Shiboli akiwa
anaenda kumsalimu kipa wa Simba SC beki wa Simba SC Novaty Lufungo
alimfanyia madhambi na mwamuzi wa mchezo huo kuamuru penati ipigwe
kuelekea langoni mwa Simba SC, huku Lufungo akizawadiwa kadi nyekundu.
Sabo aliifunga penati hiyo kwa ustadi
mkubwa na kuiandika Coastal union goli la pili na kupelekea Simba SC
kukubali kichapo cha goli 2-1 toka kwa Coastal union.
Bingwa wa michuano hii ndio atakae iwakilisha Tanzania bara katika michuano ya kombe la shirikisho la soka
Africa (CAF confederation cup) mwakani.
Droo ya Nusu Fainali inatarajiwa kufanyika kesho Saa 3:00 usiku moja kwa moja kupitia chaneli ya Azam Two ya Azam TV.
Robo
nyingine za michuano hiyo iliyoanza mwishoni mwa mwaka jana kwa
kushirikisha timu 64, Azam FC iliitoa Prisons kwa kuifunga 3-1, Mwadui
FC iliitoa Geita Gold kwa kufunga 3-0 na Yanga SC iliwafunga Ndanda FC
2-1.
Ikumbukwe bingwa wa Kombe la ASFC ataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.
Kikosi
cha Simba kilikuwa; Vincent Angban, Emery Nimubona, Mohammed Hussein
‘Tshabalala’, Hassan Isihaka, Novaty Lufungo, Justice Majabvi/Hamisi
Kiiza dk47, Hassan Kessy, Jonas Mkude, Danny Lyanga, Ibrahim Hajibu na
Said Ndemla/Awadh juma dk46.
Coastal
Union; Fikirini Bakari, Said Jeilan/Ally Ahmed ‘Shiboli’ dk46, Mbwana
Hamisi ‘Kibacha’, Abdulhahlim Humud, Twaha Ibrahim ‘Messi’, Godfrey
Wambura, Juma Mahadhi na Tumaini Mosha.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatatu, 11 Aprili 2016
Home
/
Unlabelled
/
MNYAMA UAWAWA TAIFA, APIGWA 2-1 NA COASTAL, DROO YA NUSU FAINALI ASFC KUFANYIKA KESHO LIVE
MNYAMA UAWAWA TAIFA, APIGWA 2-1 NA COASTAL, DROO YA NUSU FAINALI ASFC KUFANYIKA KESHO LIVE
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni