Kwa hivi sasa Duniani jina la Mbrazil Neymar haliwezi kukosekana miongoni mwa wachezaji bora kipindi hiki.
Wanamichezo wengi wanaamini kwamba aina ya wachezaji kama Neymar huvuna pesa nyingi kwenye mishahara yao katika vilabu wanavyochezea, lakini kupitia mtandao wa Football Leaks imefahamika mshahara halisi wa Neymar anaolipwa na FC Barcelona.
Football leaks, ambao wamekuwa wakivujisha siri mbalimbali za mikataba ya soka kama ya Gareth Bale, Sergio Aguero na Anthony Martial, leo wameivujisha document iliyosainiwa na Neymar wakati akijiunga na Barca 2103.
Cha kushangaza kwenye mkataba huo ni kuona mshahara wa Neymar ni mdogo kuliko wanaopokea wachezaji wa kawaida katika Premier League aina ya Ashley Young.
Mshahara wa Neymar unaonekana kuwa ni €5million kwa wiki ambao kwa hesabu za haraka haraka anachukua £77,000 kwa
Mkataba huo pia unahusisha vipengele vifuatavyo.
1. Ikiwa Neymar atacheza asilimia 60 ya mechi zote – Barcelona watalazimika kumlipa kiasi cha €1,062,500 za bonasi
2. Kila mara Barcelona wanapofuzu kucheza Champions League, nahodha huyo wa Brazil anavuna €637,500. Mkataba unasisitiza kwamba malipo haya yatafanyika pale tu Barca atakapoingia moja kwa moja kwenye michuano hiyo na sio kucheza mechi za kufuzu.
3. Kila klabu ya Catalunya itakapokuwa ikifuzu kucheza hatua inayofuata baada ya makundi, Neymar anavuna kiasi cha €425,000.
4. Neymar ana bonasi nyingine kubwa kila Barca wanaposhinda taji. La Liga anachukua €637,500; Champions League: €850,000 na Copa del Rey: €850.000.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni