Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya vodacom
Yanga SC wametoka sare na Al-ahly ya Misri katika mchezo wa klabu
bingwa Afrika uliochezwa katika uwanja wa Taifa hii leo.
Katika mchezo huo wa kwanza wa mzunguko
wa pili wa klabu bingwa Afrika, Yanga SC walianza mchezo kwa kasi na
katika dakika ya kwanza walifanikiwa kupata kona ambayo haikuzaa matunda
yoyote kwa yanga sc.
Al-ahly wakicheza soka la taratibu na
pasi fupi fupi walikuwa wa mwanzo kupata goli kupitia kwa Amri Gamal
katika dakika ya 11 ya mchezo
Kuingia kwa goli hilo yanga sc waliendelea kutumia mipira mirefu, kusaka goli la kusawazisha, huku Al-ahly wakipoza mchezo huo.
Yanga walisawazisha goli hilo katika
dakika ya 19 baada ya mlinzi wa Al-ahly, Ahmed Sayed kujifunga katika
harakati ya kuokoa krosi ya Boubacry na kupeleka dakika 45 za mwanzo
kumalizika kwa sare ya goli 1-1.
Katika kipindi cha pili Al-ahly walianza
kwa kutawala mpira na katika dakika ya 48 amanusura waandike goli la
pili kufuatia shuti la mshambuliaji wa Al-ahly kugonga mwamba.
Kocha wa yanga Pluijim alimpumzisha
Deusi Kaseke na nafasi yake kuchukuliwa na Geofrey Mwashuiya, huku
akimtoa Amisi Tambwe na kuingia Saimon Msuva kitendo kilichopelekea
Yanga kurejesha utawala wake wa mchezo.
Katika dakika ya 78 kipa wa yanga Ally
Mustapha Bathezi aliumia na nkukimbizwa hospitali, na nafsi yake
kuchukuliwa na Deogratius Munish 'Dida' na mpaka dakika 90 zinakamilika
Yanga SC 1-1 Al-ahly.
Kwa
matokeo, Yanga italazimika kwenda kushinda ugenini ili kutimiza ndoto
za kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa mara ya pili katika
historia yao baada ya mwaka 1998.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumamosi, 9 Aprili 2016
YANGA YAWAVIMBIA WAARABU, WATOKA SARE 1-1, NGOMA BADO MBICHI
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni