STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 15 Aprili 2016

HII NI NAFUU KWA YANGA WAKIENDA KWENYE MECHI KULE MISRI KWA WAARABU



Mashabiki sugu wa Al Ahly maarufu kama Ultras wakishangilia katika mchezo wa kwanza jijini Dar. ( Picha Soka360)
Mashabiki sugu wa Al Ahly maarufu kama Ultras wakishangilia katika mchezo wa kwanza jijini Dar. 

Pambano la marudiano kati ya Al Ahly ya Misri na Yanga litachezwa kwenye uwanja wa Borg Al-Arab wenye uwezo wa kubeba watazamaji 86,000 lakini Chama cha Kandanda nchini Misri kimesema ni mashabiki wasiozidi 15,000 watapewa tiketi za kuingia uwanjani kutazama mchezo huo.

Mkurugenzi mtendaji wa Chama cha Kandanda cha Misri ( EFA), Tharwat Swilan  amethibitisha tiketi za mchezo huo hazitauzwa kwa mashabiki kwa njia ya kawaida.

Mashabiki watajaza fomu za maombi ya tiketi mtandaoni kisha bahati nasibu kuchezeshwa kwa ajili ya kuchagua mashabiki watakaotumiwa mualiko wa kuingia uwanjani.

Yanga itakuwa mgeni wa Al Ahly katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaochezwa siku ya Jumatano. 

Wawakilishi wa Tanzania wanahitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya kuanzia mabao 2 ili kuweza kusonga mbele na kufuzu kwa hatua ya makundi kwa mara ya pili.

source: soka360

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox