Mashabiki sugu wa Al Ahly maarufu kama Ultras wakishangilia katika mchezo wa kwanza jijini Dar.
Mkurugenzi mtendaji wa Chama cha Kandanda cha Misri ( EFA), Tharwat Swilan amethibitisha tiketi za mchezo huo hazitauzwa kwa mashabiki kwa njia ya kawaida.
Mashabiki watajaza fomu za maombi ya tiketi mtandaoni kisha bahati nasibu kuchezeshwa kwa ajili ya kuchagua mashabiki watakaotumiwa mualiko wa kuingia uwanjani.
Yanga itakuwa mgeni wa Al Ahly katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika utakaochezwa siku ya Jumatano.
Wawakilishi wa Tanzania wanahitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya kuanzia mabao 2 ili kuweza kusonga mbele na kufuzu kwa hatua ya makundi kwa mara ya pili.
source: soka360
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni