Klabu
ya Yanga, leo imetangaza viingilio vya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa
Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri itakayopigwa Jumamosi wiki hii jijini
Dar.
Akitaja
viingilio vya mchezo huo unaotarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Taifa,
Dar, Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro, amesema
watazamaji watakaokaa kwenye viti vya mzunguko watalazimika kulipia Sh
5000, V.IP B na C ni Sh 25, 000 huku V.I.P A ikiwa ni Sh 30,000.
“Tumetangaza
mapema viingilio kwa ajili ya kutoa fursa kwa wapenzi na mashabiki wa
Yanga na wapenda soka kwa jumla kuweza kujipanga mapema kuja kushuhudia
mchezo huo,” alisema Muro.
Katika
hatua nyingine, Muro alisema mchezo huo utaonyeshwa kwenye runinga
lakini wale watakaopata fursa ya kuuona ni wakazi waliopo nje ya Jiji la
Dar es Salaam pekee na nje ya Tanzania.
Tayari
Al Ahly wameshawasili nchini mapema leo wakiwa na kikosi chao kamili na
mchezo huo unatarajiwa kuanza majira ya saa 10 jioni, huku Yanga
ikiendelea kujifua Kisiwani Pemba kwa ajili ya mechi hiyo inayotazamiwa
kuwa kali na ya kusisimua.
Chanzo: Saleh Jembe
Chanzo: Saleh Jembe
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni