STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 6 Aprili 2016

KIPORO CHA AZAM KIMECHACHA TENA, 2-2 NA NDANDA, COASTAL HOI, ANGALIA MSIMAMO ULIVYO

Kiporo cha mabingwa wa klabu bingwa Afrika mashariki na kati Azam FC kimechahcha hii leo baada ya kulazimishwa sare ya goli 2-2 na Ndanda FC katika mchezo wa ligi kuu ya vodacom uliochezwa hii leo katika uwanja wa Azam complex.
Katika mchezo huu wa leo Azam FC waliuwanza mchezo vyema na katika dakika ya 16 Ramadhhan Singano kuiandika Azam FC goli la kwanza.

Kuingia kwa goli hilo lilipelekea Azam Fc kutawala mchezo kabla ya Dider Kavumbagu kufunga goli la pili katika dakika ya 42 akimalizia kazi nzuri ya Waziri Salum na kupeleka mchezo kwenda mapumziko Azam wakiwa mbele kwa goli 2-0.


Kipindi cha pili, Ndanda walizinduka na kusawazisha mabao yote – akianza Atupele Green kwa penalti dakika ya 51 baada ya kipa Aishi Manula kuchezea rafu Paul Ngalema ndani ya boksi na refa Ahmad Simba wa Kagera kutenga tuta.

Zikiwa zimesalia dakika mbili mchezo kumalizika, Ahmed Msumi alyetokea benchi kipindi cha pili aliifungia Ndanda bao la kusawazisha dakika ya 88 baada ya kufumua shuti la mbali kutokea pembeni na kumbabatiza beki wa Azam Agrey Morris na kutinga wavuni.



Kwa matokeo hayo Azam FC wanajiongezea pointi nyingine moja na kufikisha pointi 52 wakiwa nyuma kwa pointi 5 toka kwa vinara Simba SC na pointi 1 toka kwa Yanga SC.



Kikosi cha Azam FC kilikuwa: Aishi Manula, Erasto Nyoni, Waziri Salum/David Mwantika dk46, Aggrey Morris, Racine Diouf/Mudathir Yahya dk46, Serge Wawa, KIpre Bolou, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Didier Kavumbagu/John Bocco dk70, Kipre Tchetche na Ramadhani Singano ‘Messi’. 

Ndanda FC: Jeremiah Kisubi, Aziz Sibo, Paul Ngalema, Hemed Khoja, Cassian Ponera, William Lucian, Salum Minelly, Masoud Ally/Burhan Rashid dk20, Omary Mponda/Ahmad Msumi dk85, Atupele Green na Kigi Makassy.

Na katika mchezo mwingine


Jahazi la wagosi wa kaya Coastal union limeendelea kuzama hii leo baada ya kupokea kichapo cha goli 2-0 toka kwa Majimaji FC katika mchezo wa ligi kuu ya vodacom uliochezwa hii leo katika uwanja wa Majimaji mkoani Songea.

Kwa mujibu wa matokeo hayo coastal union iliyobakiwa na michezo mitano, inaitaji ushindi katika michezo yote hiyo, ili ijihakikishie kubaki ligi kuu ya vodacom kwa msimu ujao.


MSIMAMO WA LIGI KUU BAADA YA MCHEZO WA LEO

RnTimuPWDLFAGdPts
1SIMBA SC24183343133057
2YANGA22165154124253
3Azam FC23157140162452
4MTIBWA SUGAR23126528161242
5T. PRISONS25101052220240
6MWADUI FC249782321234
7STAND UNITED25104112222034
8MAJIMAJI FC2586111833-1530
9NDANDA FC2551282226-427
10MBEYA CITY2576122733-627
11TOTO AFRICANS2569102334-1127
12KAGERA SUGAR2567121928-925
13JKT RUVU2466122433-924
14MGAMBO SHOOTING2558122031-1123
15AFRICAN SPORT2655161030-2020
16Coastal Union2647151537-2219



 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox