SHIRIKISHO
la Soka Tanzania (TFF) limeahidi kuwachukukliwa hatua maofisa wake
waliohusika katika mpango mchafu wa kuisaidia timu moja ya Ligi Daraja
la Kwanza Tanzania Bara.
Sauti
za kurekodiwa za Maofisa wa TFF wakiwa kwenye kikao cha pamoja na
viongozi wa timu moja ya daraja la kwanza na zimekuwa zikisambazwa
kwenye mitandao tangu jana.
Na
Taarifa ya TFF leo imesema kwamba pamoja na kwamba taarifa hizo
zilizosambazwa hazihusiani na kesi ya kupanga matokeo iliyoamuliwa siku
ya tarehe 03/04/2016, TFF inachunguza kubaini uhalisia (authenticity) wa
taarifa hizo na itachukua hatua kali sana kwa watumishi wa shirikisho
na viongozi wa timu husika watakaobainika kushiriki vitendo vilivyo
kinyume na maadili ya mpira wa miguu.
TFF
imekwishaweka bayana nia ya kupambana na yeyote atakayehusika katika
upangaji matokeo na uhalifu mwingine unaoharibu ustaarabu wa mpira kwa
njia yoyote ile.
TFF
pia linatoa onyo kwa baadhi ya viongozi, watumishi wa TFF na wadau wa
mpira wa miguu kwa ujumla wanaotumia majina ya viongozi wa juu wa TFF
katika kufanikisha mipango yao kwa manufaa binafsi.
TFF imewaomba wapenda mpira wa miguu kuwa watulivu na waangalifu wakati suala hili linashughulikiwa.
Aidha,
kuhusu hukumu ya Kamati ya Nidhamu ya TFF ni muhimu ikaeleweka wazi
kwamba zipo taratibu za kukata rufaa kwa mujibu wa kanuni ili upande
usioridhika na maamuzi yanayotolewa uweze kuhoji maamuzi husika.
Ni
vema tukaacha kamati huru zifanye kazi zake kwa mujibu wa taratibu.
Kutoa hukumu mtaani au kwenye vyombo vya habari kunaweza kuwanyima haki
wanaostahili na kutengeneza kichaka cha kujificha watenda maovu.
SIKILIZA SAUTI HAPO CHINI WAHESHIMIWA WAKISHAWISHI MTONYO UTOLEWE
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 6 Aprili 2016
Home
/
Unlabelled
/
TFF KUCHUKUA HATUA KALI JUU YA MAAFISA WAKE KWA UPANGAJI MATOKEO FDL, IPO HAPA SAUTI WAHESHIMIWA WALIVYOKUWA WANATAKA PESA
TFF KUCHUKUA HATUA KALI JUU YA MAAFISA WAKE KWA UPANGAJI MATOKEO FDL, IPO HAPA SAUTI WAHESHIMIWA WALIVYOKUWA WANATAKA PESA
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni