STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 6 Aprili 2016

TFF KUCHUKUA HATUA KALI JUU YA MAAFISA WAKE KWA UPANGAJI MATOKEO FDL, IPO HAPA SAUTI WAHESHIMIWA WALIVYOKUWA WANATAKA PESA

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeahidi kuwachukukliwa hatua maofisa wake waliohusika katika mpango mchafu wa kuisaidia timu moja ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.
 
Sauti za kurekodiwa za Maofisa wa TFF wakiwa kwenye kikao cha pamoja na viongozi wa timu moja ya daraja la kwanza na zimekuwa zikisambazwa kwenye mitandao tangu jana. 

Na Taarifa ya TFF leo imesema kwamba pamoja na kwamba taarifa hizo zilizosambazwa hazihusiani na kesi ya kupanga matokeo iliyoamuliwa siku ya tarehe 03/04/2016, TFF inachunguza kubaini uhalisia (authenticity) wa taarifa hizo na itachukua hatua kali sana kwa watumishi wa shirikisho na viongozi wa timu husika watakaobainika kushiriki vitendo vilivyo kinyume na maadili ya mpira wa miguu.

TFF imekwishaweka bayana nia ya kupambana na yeyote atakayehusika katika upangaji matokeo na uhalifu mwingine unaoharibu ustaarabu wa mpira kwa njia yoyote ile.

TFF pia linatoa onyo kwa baadhi ya viongozi, watumishi wa TFF na wadau wa mpira wa miguu kwa ujumla wanaotumia majina ya viongozi wa juu wa TFF katika kufanikisha mipango yao kwa manufaa binafsi.

TFF imewaomba wapenda mpira wa miguu kuwa watulivu na waangalifu wakati  suala hili linashughulikiwa.

Aidha, kuhusu hukumu ya Kamati ya Nidhamu ya TFF ni muhimu ikaeleweka wazi kwamba zipo taratibu za kukata rufaa kwa mujibu wa kanuni ili upande usioridhika na maamuzi yanayotolewa uweze kuhoji maamuzi husika.

Ni vema tukaacha kamati huru zifanye kazi zake kwa mujibu wa taratibu. Kutoa hukumu  mtaani au kwenye vyombo vya habari kunaweza kuwanyima haki wanaostahili na kutengeneza kichaka cha kujificha watenda maovu.

SIKILIZA SAUTI HAPO CHINI WAHESHIMIWA WAKISHAWISHI MTONYO UTOLEWE 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox