STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 11 Julai 2016

SHAVUUU: CR7 KIROHO SAFI AMKABIDHI LUIS NANI TUZO YAKE ALIYOSHINDA JANA.....


NAHODHA wa timu ya Taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo ameuonyesha umma kuwa yeye ni mtu wa ajabu baada ya kuamua kumkabidhi kiungo Luis Nani kiatu cha Silva alichopewa kama zawadi baada ya kufunga mabao matatu na kusaidia upatikanaji wa mengine mawili kwenye Michuano ya EURO 2016.
Kiatu cha dhahabu katika michuano hiyo iliyomalizika jana kwa Ureno kuibuka mabingwa kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Ufaransa, kilinyakuliwa na Antoine Griezmann aliyefanikiwa kufunga mabao sita na kusaidia upatikanaji wa mengine mawili.
Baada ya kukabidhiwa kiatu hicho,  Nani aliyechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa ubingwa huo aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram maneno ya kumshukuru Ronaldo huku akimtaja kuwa zaidi ya nahodha na ni bingwa wa ukweli.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox